Pages

Thursday, September 1, 2016

TUKIO LA KUPATWA KWA JUA - WANAFUNZI NA WALIMU WASHUHUDIA

LEO Septemba Mosi 2016, wakati mamia ya watu wa mji wa Mbeya (Rujewa) wakishuhudia tukio la kupatwa kwa jua kwa karibu asilimia tisini na nane (98%), huku wilaya ya lushoto - tanga , hususani shule ya sekondari lushoto, wanafunzi na walimu pia walipata fursa hii adhimu ya kushuhudia tukio la kisayansi na kijiografia la kupatwa kwa jua.


Ilikuwa takribani majira ya saa tano hadi saa sita mchana, wasaa ambao kwa maeneo haya (shuleni) ndipo tukio hilo lilipata kuonekana, ingawaje lilisukwasukwa na wingi wa mawingu.







Tukio hili la kupatwa kwa jua, ni somo muhimu (kwa njia ya kushuhudia na kuona mubashara pasina shaka wala kuhadithiwa) walilopata kuona na kujifunza wanafunzi wetu, na kujiongezea maarifa Zaidi hasa katika somo la jiografia.

























Ikumbukwe kuwa tukio kama hilo la kupatwa kwa jua lilitokea Julai 31,1962 takribani miaka 50 iliyopita na tukio lingine lilitokea Aprili 18, 1977, na wataalamu wa anga wanabainisha kuwa tukio kama hilo litatokea tena hapa nchini Mei 21, 2031.

No comments:

Post a Comment